Taasisi inatoa huduma ya kuhifadhi Hazina na rasilimali za Taifa na kuhakikisha kwamba rasilimali hizi zinahifadhiwa kwa njia bora na salama, kwa kuzingatia viwango na miongozo ya kimataifa ili ziweze kudumu kwa muda mrefu.
Taasisi inajukumu la kuhaulisha nyaraka na kumbukumbu kutoka kwenye mfumo wa makaratasi na kuziweka katika mfumo wa kielektroniki. Huduma hii inarahisisha upatikanaji, uhifadhi na usimamizi wa kumbukumbu kwa ufanisi.
Taasisi ininajukumu la uhuishaji wa nyaraka ili kuhakikisha zinaendelea kudumu kwa muda mrefu zaidi,pamoja na kunatoa miongozo ya utunzaji na matengenezo ya nyaraka zote zilizoathirika na ubora kutokana na matumizi ya muda mrefu.
Taasis inatoa huduma za utafiti na ushauri hutolewa kwa watafiti wenyeji na wageni. Huduma hizo ni pamoja na miongozo na taratibu za kufanya tafiti au taarifa muhimu zinazohitajika.
Nyaraka na Kumbukumbu ni rasilimali muhimu na ya kipekee (unique and irreplaceable) inayohitaji kutunzwa na kuendelezwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na baadae. Mbali ya kuwa ni utambulisho wa Taifa, nyaraka na kumbukumbu ni msingi mkuu wa Utawala Bora wa Sheria na Uwajibikaji. Aidha, hazina hii inatoa mchango mkubwa katika kujenga demokrasia,kuondoa rushwa, unyanyasaji, ubadhirifu wa mali, dhulma na vita dhidi ya umasikini.
Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu imeanzishwa na inatekeleza majukumu yake kupitia Sheria ya Kuanzishwa kwa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar Nam. 3, 2008. Jukumu kuu la Taasisi ni kutunza na kuhifadhi kumbukumbu na nyaraka za Serikali kama Urithi wa Taifa. Pia kusimamia kumbukumbu zote zinazozalishwa na kuhifadhiwa katika taasisi na mashirika ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, pamoja na taasisi na mashirika ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ofisi zake zilizopo Zanzibar.